RAIS MAGUFULI ASHANGAA PAPAI, FENESI NA MBUZI KUKUTWA NA CORONA...ASHTUKIA MCHEZO WA AJABU


CORONA
Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ameeleza kushangazwa kufuatia sampuli za Papai, Mbuzi kukutwa na Virusi vya Corona baada ya kupimwa kwenye Maabara kuu ya Taifa.

Rais Magufuli amesema hayo wakati akimuapisha Waziri wa Katiba na Sheria Mwigulu Nchemba Chato mkoani Geita ambapo amemtaka kwenda kufanya uchunguzi kwenye suala la maabara ya Taifa.

"Waziri nimekuapisha leo itabidi wewe kwa kushirikiana na Wizara ya Afya mkafanye uchunguzi kwenye masuala flani katika maabara ya taifa ya Tanzania iliyokuwa inahusika kupima Corona kuna Controlversal nyingi za ajabu,tuliona walikuwa wanatoa matokeo chanya..positive positive tu mara nyingi.

Nilizungumza na vyombo vya ulinzi na usalama na nikatoa maelekezo,hebu nendeni mkacheki hivi vipimo vikoje,hivyo vifaa vikoje na mara nyingi nimekuwa nikisisitiza kwamba si kila kitu unachopewa lazima kiwe kizuri..wanaweza kutumika watu,vinaweza kutumika hivyo vifaa lakini pia hii inaweza kuwa sabotage tu kwa sababu hii ni vita"- Amesema Rais Magufuli.

Ninamshukuru sana Katibu Mkuu Mpya Prof. Mchembe ,wameenda na kufanya mambo yafuatayo kwa kutumia na vyombo vyetu pia:

"Tulichukua Sample za Mbuzi,tukachukua sample za kondoo,tukachukua sampo za papai,tukachukua sampo za Oil ya gari na sample za vitu vingine mbalimbali tukavipeleka pale kwenye Maabara bila wao kujua na tukazipa majina..Sample ya Oil iliyotoka kwa gari tuliipa jina la Jabir Hamza mwenye miaka 30,ile ilileta Negative,tulipoleka sample ya Fenesi ambalo tulilipa jina la Sarah Samwel (45) matokeo yake yalikuwa Unconclusive,tulipopeleka sampo ya papai tukalipa jina la Elizabeth Anne (26) papai lile lilikuwa positive maana yake lilikuwa na Corona.

"Tulipeleka sample ya ndege Kware majibu yakawa positive,tumepeleka Sungura ikawa Undetermined,tumechukua mbuzi akawa Positive,tukachukua kondoo akawa Negative nk.
Sasa umepeleka sample ukamwambia huyu ni binadamu halafu ikaleta positive kwamba ina Corona maana yake yale mapapi yote yale yangewekewa Isolation,ukipeleka mbuzi wa sample nao wakawa positive maana yake mbuzi wote tulionao au huyo aliyepelekwa naye apelekwe Isolation,ukipeleka Fenesi likawa positive maana yake makamasi kamasi yake yale ambayo tuliyapa jina la Elizabeth nayo mafenesi yalitakiwa yawekwe Isolation", ameeleza Rais Magufuli.

"Kwa hiyo ukishagundua hivi lazima ujue kuna mchezo wa ajabu unafanyika kwenye vipimo hivi...kwamba kuna mambo ya ajabu yanafanywa katika nchi hii..Either Wahusika wa Maabara 'Laboratory' ile wamenunuliwa na Mabeberu,Either hawana utaalamu which is not True kwa sababu maabara hii imetumika sana kwenye magonjwa mengine!, Either zile sample zinazoletwa kwa sababu mpaka Reagent zinatoka nje,mpaka zile Swap..vile vipamba vinatoka nje..lazima kuna kitu flani kinafanywa

Na kama mapapai yanaonekana Positive yana Corona basi WHO inatakiwa ifanye kazi kubwa katika haya,na kama mbuzi nao wana Corona,na kama hawajajua kuwa hii Corona ina affect binadamu,mbuzi hata miti basi wanasayansi hatujafanya cha kutosha katika hili...Kwa hiyo kutokana na taarifa hizi zilizonazo lazima  kuna watu wameambiwa Positive wakati siyo wagonjwa wa Corona na inawezekana wengine wakafa kwa hofu..Papai lile lipo halijafa, lipo tu linaiva, mbuzi yule yupo tu wala hajafa, fenesi lile lipo labda lije lioze tu kwa muda wake lakini yale ni Positive na vitu vingine",ameongeza Rais Magufuli.

Kutokana na hali hiyo Rais Magufuli amesema licha ya kwamba Corona ipo amewataka Watanzania kutokuwa na hofu kutokana na Corona

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post