WAGONJWA WA CORONA NCHINI KENYA WAFIKA 465

Wizara ya afya nchini Kenya imethibitisha maambukizi mapya 30  ya virusi vya corona hii ni baada ya sampuli 883 kufanyiwa vipimo katika muda wa saa 24 na kufanya idadi ya walioambukizwa kufikia  465.


Naibu waziri wa afya Dk Rashid Aman anasema kuwa  19 ni wagonjwa kutoka Mombasa, 8 jijini Nairobi wawili kaunti ya Bungoma na kimoja kaunti ya Kitui.

Watu wawili zaidi aidha wamefariki kaunti ya Mombasa  kutokana na virusi hivyo na kufikisha waliofariki nchini Kenya kuwa 24 na idha waliopona ni  167 baada ya watu 15 zaidi kuruhusiwa kuondoka hospitalini.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post