MBUNGE AZZA HILAL ACHANGIA NDOO SITA ZA RANGI UJENZI OFISI YA CCM TAWI LA BUGANZO JIMBO LA MSALALA


Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM) ametekeleza ahadi ya kuchangia ndoo sita za rangi kwa ajili ya ofisi ya Chama Cha Mapinduzi tawi Buganzo kata ya Ntobo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala (Jimbo la Msalala).

Akikabidhi ndoo hizo kwa Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kahama,Thomas Myonga leo Jumamosi Mei 9,2020, Mhe. Azza amesema mchango huo ni kuunga juhudi za wanachama wa CCM ambao wamejenga ofisi ya chama.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kahama,Thomas Myonga amemshukuru Mbunge Azza Hilal kwa kutimiza ahadi yake ya kusaidia ujenzi wa ofisi hiyo ya chama.
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM) akimkabidhi ndoo sita za rangi Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kahama,Thomas Myonga (wa pili kulia) kwa ajili ya ofisi ya Chama Cha Mapinduzi tawi Buganzo kata ya Ntobo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala leo Jumamosi Mei 9,2020. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Ndoo sita za rangi Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kahama,Thomas Myonga zilizotolewa na Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Shinyanga Mhe. Azza Hilal Hamad (CCM) kwa ajili ya ofisi ya Chama Cha Mapinduzi tawi Buganzo kata ya Ntobo katika halmashauri ya wilaya ya Msalala

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527