WALIOFARIKI KWA CORONA MAREKANI WAFIKIA 45,343.....MAAMBUKIZI YAFIKA 819,175


Marekani imeendelea kuongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya vifo vinavyotokana na corona Duniani ambapo hadi mchana huu idadi ya waliofariki  imefika 45,343.


Marekani pia inaongoza kwa visa, vimefikia 819,175  na wamepona 82,973

Jana Jumanne Marekani ilirekodi vifo 2,750 kwa siku licha ya takwimu mpya kuonesha maambukizi ya kila siku yanapungua nchini humo. 

Majimbo ya New Jersey, Pennsylvania na Michigan kila moja liliripoti vifo vya zaidi ya watu 800 kwa siku, huku jimbo la New York lililo kitovu cha mlipuko wa virusi vya corona nchini Marekani lilirekodi vifo vya watu 481.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527