RAIS WA ZAMANI WA SUDAN OMAR AL-BASHIR AOMBA KUHAMISHWA GEREZA BAADA YA MSAIDIZI WAKE WA ZAMANI KUPATA CORONA


Rais wa zamani wa Sudan Omar al-Bashir ametaka kuhamishwa gereza kufuatia habari kwamba mmoja wa wasidizi wake wa zamani ameambukizwa virusi vya Corona.


Bashir amefungwa katika gereza la Kober pamoja na ofisa wa zamani wa Wizara ya mambo ya ndani Bw. Ahmed Hrouna, ambaye alihamishwa katika hospitali ya gereza baada ya kuthibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona. 

Mkuu wa timu ya ulinzi wa Bashir Bw. Mohamed al-Hassan al-Amin amesema, hali ya Bw. Haroun si mbaya sana.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527