ASKARI POLISI AKUTWA AMEFARIKI DUNIA MTARONI


Askari wa kituo cha polisi Kia, Sajenti Juma Ango amekutwa akiwa ametupwa mtaroni mita chache kutoka kituo cha polisi Hai Mjini mkoani Kilimanjaro.

Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya amesema watu waliokuwa wakifyeka majani kandokando ya barabara ndiyo waliokutana na mwili huo.

Sabaya amesema mwili huo umekutwa ukiwa na na jeraha kubwa kisongoni na kwamba alikuwa amepigwa na kitu chenye ncha kali.

"Taarifa zinasemekana alikuwa na askari wenzake jana hadi saa nane usiku maeneo ya Msami,"amesema Sabaya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post