WENYE VIRUSI VYA CORONA TANZANIA WAFIKA 24

Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametangaza uwepo wa wagonjwa wengine wapya wanne wa maambukizi ya virusi vya corona 

Waziri Ummy ametangaza leo Jumatatu Aprili 06, 2020 katika taarifa yake kwa vyombo vya habari inayoelezea mwenendo wa hali ya corona nchini

Amesema kuwa kati ya wagonjwa hao wanne, wawili wanatoka Tanzania Bara na wawili wanatoka Zanzibar

 “Wizara ya Afya imethibitisha kuwepo kwa kesi mpya nne za maambukizi ya virusi vya corona (COVI-19) zilizopatikana Dar es Salaam, Mwanza na Zanzibar na kufanya kuwepo kwa jumla ya kesi 24 zilizoripotiwa tangu kuanza kwa ugonjwa huu nchini” imesema sehemu ya taarifa hiyo


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527