WALIOPONA VIRUSI VYA CORONA NCHINI TANZANIA WAFIKA WATANO


Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema wagonjwa wengine  2 wa Corona hapa nchini  wamepona na kufanya idadi ya waliopona kufika 5 huku kifo kikiwa ni kimoja.


Amesema kati ya wagonjwa hao, Dar es Salaam - 1 na Arusha - 1.  Hivyo sasa Mkoa wa Arusha hauna mtu mwenye maambukizi ya COVID19. 

Waziri Ummy amewataka Watanzania waendelee kuzingatia maelekezo ya Wataalam wa Afya ikiwemo kuepuka mikusanyiko na misongamano  isiyo ya lazima


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post