RAIA WANNE WA KIGENI WALIOINGIA NA MAFUA UGANDA WATENGWA KWA HOFU YA VIRUSI VYA CORONA

Raia wanne wa kigeni waliowasili nchini Uganda na dalili za virusi vya corona wametengwa katika hospitali ya Entebbe, Waziri wa afya amethibitisha.


Bila ya kutaja uraia wao, afisa mahusiano wa waziri wa afya bwana Emmanuel Ainebyoona alisema kuwa raia hao wamechukuliwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Entebbe.

"Sampuli ya vipimo vyao vimepelekwa katika kituo cha utafiti wa virusi nchini humo (UVRI). Na tutaitaarifu umma " gazeti la Daily Monitor limemnukuu

Wizara ya afya imewataka wananchi kuwa watulivu na kufuata hatua za kujikinga na ugonjwa wa corona kwa sababu hakuna udhibitisho wa kuwa virusi hivyo vimeingia nchini humo.

-BBC


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527