MAALIM SEIF SHARIF HAMAD ACHAGULIWA KUWA MWENYEKITI MPYA WA CHAMA CHA ACT WAZALENDO


Maalim Seif Sharif Hamad amechaguliwa kuwa mwenyekti mpya wa chama cha ACT- Wazalendo huku Zitto Kabwe akitetea nafasi kiongozi wa chama hicho kwa mara ya pili mfululizo katika uchaguzi uliofanyika jana Machi 14, 2020.

Kwa matokeo hayo Maalim Seif ambaye pia ni mshauri mkuu wa ACT-  Wazalendo anakuwa mwenyekiti wa pili wa chama hicho tangu kuanzishwa kwake mwaka 2014.

Maalim Seif na Zitto Kabwe ambaye ni mbunge wa Kigoma Mjini walichaguliwa usiku wa kuamkia leo Jumapili Machi 15, 2020 katika mkutano mkuu wa pili wa chama hicho uliokuwa na ajenda mbalimbali ikiwemo ya uchaguzi wa viongozi wa nafasi ya uenyekiti na kiongozi wa ACT- Wazalendo.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527