MSANII KENNY ROGERS AFARIKI DUNIA


Msanii Kenny Rogers (81) raia wa Marekani, amefariki Dunia akiwa nyumbani kwake.

Kwa mujibu wa familia yake kifo cha Msanii huyo ni cha kawaida na wala hakihusishwi na jambo lolote .

Rogers, alitamba kwa nyimbo zake nyingi zikiwemo The Gambler, Lady, Islands in the Stream na Lucille, huku akiwa ameuza rejodi zaidi ya Milioni na kushinda tuzo 3 za Grammy.

Kama muigizaji ametokea kwenye filamu ya Six Pack mwaka 1982 na katika tamthilia kadhaa maarufu za runinga kama The Gambler franchise, Christmas in America na Coward of the County.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527