![](https://www.eatv.tv/sites/default/files/styles/detailpageimg/public/news/2020/03/21/ROGGERS.jpg?itok=KwjLDHFt×tamp=1584779419)
Msanii Kenny Rogers (81) raia wa Marekani, amefariki Dunia akiwa nyumbani kwake.
Kwa mujibu wa familia yake kifo cha Msanii huyo ni cha kawaida na wala hakihusishwi na jambo lolote .
Rogers, alitamba kwa nyimbo zake nyingi zikiwemo The Gambler, Lady, Islands in the Stream na Lucille, huku akiwa ameuza rejodi zaidi ya Milioni na kushinda tuzo 3 za Grammy.
Kama muigizaji ametokea kwenye filamu ya Six Pack mwaka 1982 na katika tamthilia kadhaa maarufu za runinga kama The Gambler franchise, Christmas in America na Coward of the County.