NACTE YAFUTA USAJILI WA VYUO 7


Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi NACTE imevifutia usajili vyuo saba ambavyo vimethibitika kuendesha mafunzo bila kukidhi vigezo na utaratibu.

Akitoa taarifa hiyo mbele ya wanahabari, Mkurugenzi wa Opresheni wa NACTE, Dr Geofrey Oleke amesema lengo la kuvifutia vyuo hivyo usajili ni kutaka vikamilishe taratibu ili kutoa elimu yenye manufaa kwa Watanzania kwa kufuata misingi.

Orodha ya vyuo vilivyofutiwa usajili ni pamoja na ERA Training College - Bukoba (REG/TLF/095), Azania College of Management - Dar es Salaam (REG/BMG/021), Time School of Journalism - Dar es Salaam (REG/PWF/013), Clever College - Dar es Salaam (REG/BTP/205P) na Aces College of Economic Science - Mwanakwerekwe, Zanzibar (REG/BPT/081P).


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post