Mufti atoa tamko tukio la kuchanwa kwa Quran

Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir amewataka Waislamu nchini kuwa watulivu wakati vyombo vya sheria vikiendelea kuchukuwa hatua kwa tukio la kuchanwa kwa Quran.

Amesema kuwa kitendo cha kuchanwa kwa kwa kitabu kitukufu cha Quran kilichofanywa na Afisa Biashara wa Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro, Daniel Malaki hakihusiani na mitazamo yoyote ya kidini bali ni utashi wake binafsi

Ameongeza kuwa kitendo hicho ni cha uzalilishaji wa maneno ya Mungu yanayopelekea kuwaudhi Waislamu na kusababisha kuleta mfarakano miongoni mwa jamii.

“Niwaombe Waislamu kuendelea kuwa na subira na uvumilivu huku wakisubiri kauli za viongozi wao wa Bakwata ambao wanafuatilia kwa ukaribu kesi iliyopo mahakama kwa sasa, “amesema Mufti Zubeir.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post