TYSON AMTWANGA DEONTAY WILDER RAUNDI YA 7 NA KUWA BINGWA MPYA WA WBC


Tyson Fury ameshinda pambano lake la leo Februari 23, 2020 la uzito wa juu dhidi ya Deontay Wilder kwa TKO raundi ya 7 na kuwa bingwa mpya wa WBC.





Tyson alionyesha umahiri wake katika ulingo baada ya kumaliza ufalme wa Deontay Wilder wa miaka mitano na kuchukuwa mkanda wa WBC katika uzani mzito duniani baada ya kumwangusha binngwa huyo kwa njia ya knockout katika raundi ya saba.

Katika mechi iliochezwa katika Mecca ya ndondi mjini Las Vegas nchini Marekani raia huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 31 alimshinda mpinzani wake katika pigano ambalo ni wachache wangeweza kutabiri..

Mchanganyiko wa ngumi za kulia na kushoto ambazo Wilder amekuwa akizitumia kuwalambisha sakafu wapinzani wake zilitumika dhidi yake na kuangushwa katika raundi ya tatu na tano.

Fury alihakikisha ametimiza aliyoahidi na kubadili mbinu zake kutoka upigaji hadi mwenendo wake na kumzidia nguvu mpinzani wake ambaye hajawahi kushindwa.

Katika ukurasa wake wa Twitter, Tyson ameandika: “Nataka kusema Deontay Wilder, ameonyesha weledi wake. Amepigana hadi raundi ya saba. Yeye ni shujaa, atarejea tena kuwa bingwa. “Lakini mfalme amerejea katika kiti chake.”

Tyson Fury akizungumza na BT Sport: “Nilimwambia kila mmoja kwamba mfalme anarejea kwenye kiti chake. katika pigano langu la mwisho karibu kila mmoja alinikashifu. Nilikuwa na uzani wa chini na nilifanya mazoezi kupitiza. Mimi ni muharibifu. lakini sio vibaya kwa mwanamasumbwi.

“Natimiza ninachosema. Nilimwarifu Wilder, timu yake, na dunia nzima. Tulifanya mazoezi ya knockout.

“Ninazungumza hivi kwasababu ninaweza kutoa ushahidi wa ninachokizungumzia. Watu walinisema vibaya, waliangalia kitambi changu na upara wangu na kudhania kwamba siwezi kupigana. Alipigana kwa weledi kadiri ya uwezo wake wote Tyson Fury na kila mmoja yuko katika kipindi chake cha juu.

“Namtarajia [Wilder] aombe pigano la tatu. najua kwamba yeye ni shujaa na mimi nitakuwa na msubiri.”

Fury kisha akasema kwamba anataka pambano la tatu dhidi ya Wilder lifanyike uwanja wa Las Vegas ambao kwa sasa unajengwa na utafunguliwa hivi karibuni.

Kulingana na timu yake, Wilder amepelekwa hospitali kushonwa baada ya kujeruhiwa kwenye sikio.

-BBC


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527