IKULU YA MAREKANI YATOA TAARIFA RASMI YA SABABU ZA KUMUUA KAMANDA WA JESHI LA IRAN

Ikulu ya Marekani jana imetoa taarifa  ikisema Rais wa Marekani Donald Trump aliamuru shambulizi la droni lililomuua kamanda mkuu wa jeshi la Iran mwezi uliopita ili kujibu mashambulizi ya nyuma, licha ya madai ya awali kwamba yalitokana na tishio la hivi karibuni.

Kama inavyohitajika kisheria, serikali imetuma taarifa kwa baraza la chini la bunge la Marekani ikielezea shambulizi la Januari 2 lililomuua Qasem Soleiman katika uwanja wa ndege wa Baghdad.

 Shambulizi hilo na jibu la Iran yamezua wasiwasi na kufadhaisha baadhi ya wabunge ambao walisema Trump alifanya kosa kubwa na amewapa Wairan haki ya kushambulia.

Siku moja baada ya kutolewa kwa taarifa hiyo kwa baraza la congress, kamati ya mambo ya nje ya baraza la chini la bunge la Mrekani, imekemea kitendo  hicho cha Trump, na kupitisha  muswada wa sheria ya kuweka ukomo juu ya uwezo wa rais wa kuendelea na vita dhidi ya Iran.

Baraza hilo limepitisha mswada huo kwa kura 55 za ndiyo na kura 45 za hapana, huku wanachama 8 wa Republican wakipiga kura za ndiyo. 

Muswada huo umesisitiza kuwa rais Trump hawezi kuchukua hatua za kijeshi bila ya ridhaa ya bunge. 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527