MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA ZALETA MAAFA DODOMA


Zaidi ya nyumba 120 zimebomoka na madaraja kuharibika Wilaya ya Bahi mkoani Dodoma, kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Maeneo yaliyoathiriwa na mvua hizo ni Bahi Sokoni, Bahi Misheni, Mji mpya, Nkogwa, Mbuyuni, Uhelela, Laloi, Mugu na Nagulo.

Juzi Mkuu wa Wilaya, Mwanahamisi Mukunda akiongozana na wataalamu wa Halmashauri ya Bahi na watendaji wa vijiji, walitembelea baadhi ya wakazi walioathirika na mafuriko hayo na madaraja ambayo yameharibika.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Kijiji cha Sokoni, Sifael Mbeti alisema mvua imesababisha mito mingi kufurika na hivyo kusababisha maji kuleta madhara kwa kubomoa nyumba na madaraja.

Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Bahi Sokoni, Fredrick Kachiwile alisema zaidi ya nyumba 86 katika kijiji hicho zimebomoka.

Alisema katika Kijiji cha Uhelela taarifa za awali zinaonyesha nyumba 35 zilibomoka na katika Kijiji cha Nagulo barabara imekatika na mawasiliano ni ya shida.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nagulo, Ashery Silla alisema jumla ya nyumba 18 zimeanguka.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post