MAMIA YA WANANCHI WA IRAQ WAANDAMANA KULITAKA JESHI LA MAREKANI LIONDOKE NCHINI MWAO


Mamia ya watu wameandamana katika mji mkuu wa Iraq, Baghdad, wakidai vikosi vya Marekani viondoke Iraq.

Kiongozi mwenye ushawishi wa dhehebu la Shia Iraqi, Moqtada al-Sadr awali alitoa wito kwa mamilioni ya raia kushiriki maandamano ya Ijumaa, karibu na ubalozi wa Marekani nchini Iraq.

Vikosi vinavyoungwa mkono na Iran ni miongoni mwa wanaondamana.

Hatua ya Marekani ya kumuua kamanda wa kijeshi wa Iran, Jenerali Qasem Soleimani, Januari 3 katika uwanja wa Baghdad uliongeza uhasama

Pia aliyeshambuliwa kwa ndege ya Marekani isiyokuwa na rubani ni Abu Mahdi al-Muhandis, mmoja wa makamanda wa Iraq ambaye kundi lake la Kataib Hezbollah linaloungwa mkono na Iran pia aliuawa katika shambulio hilo.

Iran ilijibu shambulizi la mauaji ya Jenerali Soleimani kwa kutekeleza shambulizi la kombora dhidi ya kambi mbili za kijeshi za Marekani nchini Iraq.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527