KESI YA KUTEKWA MFANYABIASHARA MOHAMMED DEWJI YAPIGWA KALENDA HADI JANUARY 21


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam imepiga kalenda kesi ya kutekwa kwa mfanyabiashara Mohammed Dewji maarufu kama MO inayomkabili dereva wa taksi Mousa Twaleb na wenzake wanne ambao bado hawajakamatwa na kufikishwa mahakamani hapo.

Kesi hiyo ilitajwa jana mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Rashid Chaungu baada ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi, aliyepangiwa kusikiliza kesi hiyo kwenda likizo.

Wakili wa Serikali, Faraji Nguka, alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo aliiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa.

Hakimu Chaungu alisema kesi hiyo itatajwa Januari 21, mwaka huu na mshtakiwa ataendelea kukaa mahabusu.

Watuhumiwa wengine ambao upande wa mashtaka inawatafuta ni raia wanne wa Msumbiji na mmoja wa Afrika Kusini, wanaodaiwa kumteka bilionea huyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527