EVARISTE NDAYISHIMIYE AIDHINISHWA KUWA MRITHI WA RAIS PIERRE NKURUNZIZA


Chama tawala cha Burundi CNDD-FDD, kimemteua katibu wake mkuu kuwa mgombea wa urais katika uchaguzi mkuu wa Burundi utakaofanyika Mei 2020.


Jenerali Evariste Ndayishimiye ameidhinishwa na chama kama mrithi wa Nkurunziza wa Burundi.

Meja Jenerali Evariste Ndayishimiye ameteuliwa kama mgomba wa urais katika uchaguzi utakaofanyika Mei 2020 kumrithi Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza.

Jenerali Ndayishimiye ameteuliwa Jumapili kupeperusha bendera ya chama cha CNDD-FDD katika kikao kisicho cha kawaida kilichofanyika Gitega, mji mkuu wa kisiasa baada ya mazungumzo yaliyodumu kwa saa tatu ya chama tawala cha CNDD-FDD.

Bwana Ndayishimiye ni miongoni mwa wanasiasa mashuhuri katika siasa za Burundi waliokaribu na Pierre Nkurunziza.

Pia ni miongoni mwa waliokuwa waasi wa CNDD-FDD aliyejiunga baada ya kunusurika katika mauaji ya kikabila ya wanafunzi wa Wahutu katika chuo kikuu cha Burundi mwaka 1995.

Jenerali Ndayishimiye kwa sasa ni Katibu Mkuu wa chama cha CNDD-FDD tangu Agosti 2016.

Kabla ya kuteuliwa kwake, alikuwa Waziri wa mambo ya ndani na ulinzi wa umma.

-BBC


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527