WAZIRI MKUU WA LESOTHO PAMOJA NA MKEWE WAKABILIWA NA TUHUMA ZA MAUAJI


Waziri Mkuu wa Lesotho Thomas Thabane pamoja na mkewe, Maesaiah Thabane wanatakiwa kuhojiwa kuhusiana na mauaji yaliyotokea mwaka 2017 ya Mke wa kwanza wa Thabane, Lipolelo Thabane (58)


Lipolelo alikuwa ametengana na mume wake na alikuwa akiishi peke yake tangu mwaka 2012 ambapo aliuawa siku 2 kabla ya Thabane kuapishwa kuwa Waziri Mkuu kwa kupigwa risasi sehemu mbalimbali za mwili wake

Ushahidi wa hivi karibuni uliowasilishwa Mahakamani na Kamishena wa Polisi umebaini kwamba kulikuwa na mawasiliano ya simu katika eneo la tukio kwa kutumia namba ya simu inayodhaniwa kuwa ni ya Thabane

Waranti ya kukamatwa kwa Maesaiah Thabane ilishatolewa lakini hajaonekana hadharani kwa wiki 2 sasa, hakuna anayejua alipo na Thabane amekataa kusema alipo mke wake


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527