TAKUKURU YAZINDUA KAMPENI YA "VUNJA UKIMYA KATAA RUSHWA YA NGONO"..YAKUTANA NA WAANDISHI WA HABARI KAGERA


Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Kagera John Joseph akitoa elimu ya rushwa ya ngono kwa waandishi wa habari mkoani Kagera.

Na Ashura Jumapili - Malunde 1 blog Bukoba

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini Tanzania (TAKUKURU ) imeanzisha kampeni ya kitaifa ya" vunja ukimya kataa rushwa ya ngono "ili kutoa fursa kwa waathiriwa wa matatizo ya ngono kufunguka.

Kauli hiyo imetolewa na mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Kagera John Joseph,wakati akitoa elimu ya rushwa ya ngono kwa waandishi wa habari mkoani humo.

Joseph alisema rushwa ya ngono inamdhalilisha mtu,inasababisha magonjwa maana unaweza kujikuta unashiriki ngono na mtu ambaye ana magonjwa ya kuambukiza na kumuambukiza mwingine.

Alisema upo ulazima wa nchi na wadau mbalimbali kushirikiana ili kuweza kufichua vitendo vya rushwa ya ngono katka jamii.

Alisema matukio ya rushwa ya ngono yanafanyika kwa wingi lakini hayaripotiwi katika mamlaka husika ili ziweze kuchukua hataua stahiki.

Alisema zaidi ya matukio 391 yaliripotiwa takukuru ya kuombwa rushwa ya Ngono hapa nchini kwa mwaka 2017 Hadi 2019 na majalada 46 yalifanyiwa uchunguzi.

Alisema kuwa Takukuru Mkoa wa Kagera unampango wa kuanzisha dawati amaalumu la Rushwa ya Ngono ili jamii iweze kutambua madhara yatokanayo na rushwa ya ngono.

"Nitumie nafasi hii kuwajulisha jamii na jinsi Rushwa ya Ngono jinsi inavyo mdhalilisha mtu na inasababisha magonjwa maana huwezi jua kuwa yule anayefanya Jambo Hilo kuwa ni mgonjwa au la",alisema Joseph

Alisema kuwa Sheria ya kuzuia na Kupambana na Rushwa namba 11ya mwaka 2007 imetamka kuwa kosa chini ya Kifungu Cha 25 " Mtu yeyote ambaye kwa kutumia nafasi yake au Mamlaka yake katika kutekeleza majukumu yake anadai au analazimisha upendeleo wa Kingono au upendeleo mwingine wowote Kama kigezo Cha kutoa ajira , Kupandishwa cheo, Kutoa haki au upendeleo wowote unaotambulika Kisheria atakuwa ametenda Kosa" ,alisema Joseph.

Alisema kuwa kesi ya rushwa ya ngono zimekuwa zikishindwa mahakamani kwa kukosa ushahidi uliojitosheleza kutokana na jamii kutokuwa na elimu ya rushwa ya ngono.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527