MKUU WA MKOA WA MARA ASIMAMIA ZOEZI LA KUACHIWA HURU WAFUNGWA


Mkuu wa Mkoa wa Mara Mhe. Adam Malima akiongea na sehemu ya wafungwa 23 walioachiwa katika gereza la Musoma kati ya wafungwa 259 waliofaidika na msamaha wa Rais Mkoani humo.

Mhe Malima, ambae alikuwa ameongozana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya mkoa wa Mara (RAS) Mhe. Carlo Mthaphula,  amewataka wafungwa hao wakamlipe fadhila waliyopewa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa kwenda kutenda mema na ya maendeleo katika jamii badala ya kuanza uhalifu upya.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527