CCM YAWAONYA WALIOANZA KAMPENI ZA URAIS NA UBUNGE KABLA YA WAKATI


Katibu Mkuu wa CCM, Dkt. Bashiru Ally amewaonya wanachama wa chama hicho tawala walioanza mikakati ya kutaka kupitishwa kuwania udiwani, ubunge na urais akibainisha kuwa kufanya hivyo ni makosa.




"Watu wa namna hiyo(walioanza mapema mikakati ya kutaka kupitishwa kuwania udiwani, ubunge na urais) hawatavumiliwa kwa kuwa taratibu za kuwania uongozi, nafasi mbalimbali katika chama hicho zipo wazi na zina muda wake" Dk. Bashiru Ally, Katibu mkuu wa CCM

Ametoa kauli hiyo leo Jumanne Desemba 3, 2019 katika ziara yake kisiwani Pemba, Zanzibar wakati akizungumza na kamati ya siasa Wilaya ya Chakechake.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527