WAZIRI JENISTA AANZA ZIARA YA KUTEMBELEA VITEGA UCHUMI VYA PSSSF JIJINI DAR ES SALAAM

 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama(watatu kulia), akiongozana na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Andrew Massawe (Wanne kulia), Mkurugenzi Mkuu, Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Hosea Kashimba (Wapili kulia) na maafisa wengine wa juu wa PSSSF, mwanzoni mwa ziara ya Waziri kutembelea vitegauchumi vya Mfuko huo jijini Dar es Salaam Novemba 25, 2019.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama(katikati), akiongozana na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Andrew Massawe (kushoto), Mkurugenzi Mkuu, Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Hosea Kashimba, (kulia), wakitoka kwenye moja ya majengo ya vitegauchumi vya Mfujo huo jijini Dar es Salaam Novemba 25, 2019. Mhe. Jenista ameanza ziara ya siku mbili kutembelea vitegauchumi vya Mfukjo huo hususan majengo.
Mhe. Jenista Mhagama akisisitiza jambo baada ya kutembekea jingo la PSSSF Twin Towers katikati ya jiji la Dar es Salaam, Novemba 25, 2019.

 Mhe. Waziri akifuatana na Katibu Mkuu pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF wakitembelea jingo la PSSSF Twin Towers katikati ya jiji la Dar es Salaam Novemba 25, 2019.
 Waziri Mhe. Jenista Mhagama akizungumza wakati wa ziara hiyo huku Mkurugenzi wa Mipango na Uwelezaji PSSSF, Bw. Fortunatus Magambo akimsikiliza.
 Waziri Mhagama akimsikiliza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Andrew Massawe, wakati akifafanua jambo wakati Mhe., Waziri na msafara wake walipotembelea jingo la Quality Plaza barabara ya Nyerere jijini Dar es Salaam, ili kujionea hali ya sasa ya jingo hilo ambalo ni kitegauchumi cha PSSSF
 Waziri Mhagama akifuatana na Katibu Mkuu  Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Massawe wakati wakitembelkea jingo la PSSSF Twin Towers Novemba 25, 2019.
 Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama(kushoto),  na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Andrew Massawe (kushoto), wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu, Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Hosea Kashimba wakati Mhe. Waziri alipotembelea jingo la uwekezaji la PSSSF la Jubilee Towers barabara ya Ohio katikati ya jiji la Dar es Salaam Novemba 25, 2019. 
 Mkurugenzi Mkuu, Mfuko wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Bw. Hosea Kashimba akifafaua jambo







Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527