ALIYESHIRIKI KUTUNGA SHERIA YA KUZUIA UZINZI AFUMANIWA AKIHONDOMOLA MKE WA MTU


Mwanaume mmoja nchini Indonesia ambaye alishiriki kwa kiasi kikubwa kuandaa Muswada wa sheria ya kupinga vitendo vya uzinifu nchini humo amekamatwa akizini na mke wa mtu.

Mukhlis bin Mudammad ni mmoja kati ya wwanachama wa baraza la wanatheolojia ambalo lilisaidia kutunga sheria za Kiisilamu kupinga vitendo vya zinaa pamoja na baadhi ya makosa mengi, lakini alijikuta akicharazwa viboko 28 hadharani mbele ya kadamnasi ya watu hapo jana siku ya Alhamisi katika Mkoa wa Aceh, Besar kufuatia kufumaniwa uzinzi na Mke wa mtu.

Tukio hilo linamfanya, Mukhlis bin Mudammad mwenye umri wa miaka 46, kuwa kiongozi wa kwanza wa baraza hilo kuadhibiwa na sheria hizo baada ya kukutwa na hatia.

Mukhlis pamoja na mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 33, ambao wote wawili ni wanandoa wamepatika na hatia ya kuchepuka na kuzisaliti ndoa zao kupitia mahaka ya Mkoawa Aceh ya ekhtilat baada ya kufumwa wakifanya vitendo hivyo ndani ya gari katika fukwe mwezi uliyopita.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527