BABU WA MIAKA 71 ATANGAZA KUOA MKE WA 9...ATAFUNGA NDOA FEBRUARI 2020


 Babu Ron Sheppard akiwa na mke wake wa nane.

Ron Sheppard (71) kutokea nchini Uingereza, ni maarufu kwa jina la Muingereza ambaye mpaka sasa ameshaoa mara nane na wake zake wote ameachana nao na sasa anajipanga kuoa kwa mara ya tisa.

Ndoa hiyo ya tisa anatarajia kuifunga Februari 2020, na mwanamke anayejulikana kwa jina la Rose Hans, mwenye miaka 30, ambaye amemaliza kozi ya udaktari nchini Ghana, na anajipanga kuhamia nchini Uingereza.

Kupitia mtandao wa The Sun Online, Babu huyo amesema "Najua Rose ni mmoja wao haijalishi kama tumekutana wapi ila nachoweza kusema tuna muunganiko mzuri, umri ni namba tu sijali kama ni nusu ya miaka yangu au zaidi ana mapenzi na mimi na nampenda yeye" .

Historia yake inasema kwa sasa ni Baba wa watoto nane na ndoa yake ya kwanza alifunga akiwa na miaka 19, ilikuwa 1966, ambayo ilidumu kwa miaka miwili na kupata watoto watatu, ndoa ya pili alifunga 1973-1974, ndoa ya tatu ilikuwa 1976 na ilidumu kwa miaka mitano, ndoa ya nne ilifanyika mwaka 1982-1986.

Ndoa ya tano 1986-1997 na alipata watoto wawili wa kiume ya sita ilikuwa 1999 na alichana baada ya kumsaliti mkewe 2003, ndoa ya saba ilidumu kwa miezi 8 tu, ndoa ya nane alifunga mwaka 2004 na ilidumu kwa miaka 11 hadi kufikia 2015.

Source by The Sun Online.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527