KAULI YA MWAKINYO BAADA YA KUMCHAPA MFILIPINO ARNEL TINAMPAY


Bondia Mwakinyo akimchapa konde la uso mfilipino Arnel

Bondia Hassan Mwakinyo amesema moja ya sababu iliyopelekea yeye kumshinda Bondia Mfilipino Arnel Tinampay, ni yeye kurusha ngumi nzito huku mpinzani wake akiwa anarusha ngumi nyingi zilizokuwa nyepesi sana.

Mwakinyo ametoa kauli hiyo, baada ya kuisha kwa pambano lake usiku wa kuamkia leo lililofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam, ambapo alimchapa Mfilipino, huyo kwa alama 97-93, 98-92 na 96-96.

Mwakinyo amesema kuwa"sipigi ngumi nyepesi napiga sana madude, kilichomsaidia Mfilipino alishasoma, alikuwa ananificha ukitaka kufanya finishing na yeye anapiga."

"Najua kitu kikubwa kilichokuwa kinambeba alikuwa mvumilivu sana, ila pia Mabondia wengi huwa tunapigwa nje ya nchi kwa namna ambavyo hata yeye mwenyewe amepigwa" ameongeza Mwakinyo

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527