KIGOGO WA TACAIDS ATAKA KONDOMU KUGAWIWA BURE BAA , GESTI

Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) Dk Leonard Maboko ameeleza anavyotamani kushuhudia Serikali ikigawa kondomu bure hasa katika maeneo hatarishi ikiwemo nyumba zote wageni na kwenye baa.

Akizungumza leo Alhamisi Novemba 28, 2019 katika kongamano la kitaifa la maadhimisho ya siku ya Ukimwi duniani jijini Mwanza,Dkt. Maboko amesema ifike mahali hali ya kuzuia maambukizi isichukuliwe kama mzaha.


Amesema anatamani mwaka 2020 nyumba zote wageni, baa na maeneo mengine kondomu kugawiwa bure.

"Natamani mwakani tuweze kusambaza kondomu kila mahali ili tuweze kudhibiti ugonjwa huu, najua huko ndiko watu wanakutana na kufanya wanavyofanya lakini kama Serikali tuone namna gani tunawasaidia wale wanaoshindwa kununua," amesema Dk. Maboko

Amesema lengo ni kuzuia maambukizi mapya ya Ukimwi kwa vijana kwa maelezo kuwa kwa sasa ndio kundi linaloongoza kwa kupata maambukizi mapya.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527