HARMONIZE KUMKABILI ALI KIBA DISEMBA 8


Wasanii wa Tanzania, Alikiba na Harmonize watakutana katika jukwaa moja la tamasha la Fiesta litakalofanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam Desemba 8, 2019.

Waandaaji wa tamasha hilo Jumanne Novemba 26, 2019 wametangaza baadhi ya wasanii nchini watakaoshiriki Fiesta, wakiwemo wawili hao.

Kukutana jukwaani kwa wasanii hao kunasubiriwa kwa hamu kutokana na Harmonize kuachana na lebo ya Wasafi, hivyo mashabiki wengi kutaka kumshuhudia akitoa burudani nje ya lebo hiyo.

Alhamisi ya Oktoba 24, 2019, Harmonize alieleza jinsi alivyouza nyumba zake tatu na baadhi ya mali ili kuilipa lebo ya Wasafi Sh500 milioni kwa ajili ya kupata hakimiliki ya kutumia nyimbo zake na jina.

Alibainisha kuwa mkataba alioingia na lebo ya Wasafi inayomilikiwa na msanii Diamond Platnumz ilikuwa na kipengele cha kulipa kiasi hicho cha fedha ikiwa atavunja mkataba ili aweze kuendelea kutumia nyimbo pamoja na jina lake la kisanii.

Wakati akiwa Wasafi, Harmonize hakuwahi kushiriki tamasha la Fiesta tofauti na Ali Kiba aliyewahi kushiriki mara kadhaa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527