TAARIFA KWA UMMA; GAVANA WA BOT HAJAFUNGUA AKAUNTI YA “FACEBOOK”





Benki Kuu ya Tanzania (BoT) inapenda kuutangazia umma kwamba Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Prof. Florens Luoga, hajafungua akaunti ya mtandao wa kijamii wa Facebook, kinyume na taarifa na picha zinazojitokeza katika katika mtandao huo kwa jina lake.

Kwa taarifa hii, tunapenda kuutangazia umma kupuuza chochote kinachopatikana katika akaunti hiyo bandia inayojiita Florence Luoga, na ambayo inatumia picha mbalimbali za Gavana wa BoT kinyume cha sheria.

Aidha, Benki Kuu ya Tanzania inapenda kuwapa pole watu wote ambao kwa namna moja ama nyingine wameathirika kutokana na yote ambayo yamejitokeza katika akaunti hiyo bandia, ikiwemo kutumia jina la Gavana Luoga kutapeli na hata kutumiwa ujumbe wa matusi.

Pamoja na taarifa hii, hatua za kisheria zinaendelea kuchukuliwa ili kumbaini mhalifu huyu kwa kutumia akaunti hiyo kuchafua sifa ya Gavana Luoga katika jamii.

Tunauhakikishia umma kwamba, Gavana Luoga hajafungua akaunti kwa jina hilo na hivyo taarifa zozote zinazotolewa kwenye akaunti hiyo ya Facebook hazina uhusiano wowote na Prof. Florens Luoga.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527