BASHE AMLILIA MKURUGENZI MSTAAFI IDARA YA USALAMA WA TAIFA

Naibu Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe amesema, aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS), Apson Mwang’onda (75) alikuwa msaada mkubwa kwake kwenye safari ya kisiasa na uongozi.


Kupitia ukurasa wake wa Twitter, ameandika  kuwa, mzee Mwang'onda alikuwa baba, rafiki, mshauri, na kiongozi.

"Nimepokea kwa masikitiko na uchungu, taarifa za kifo cha baba yetu, rafiki, mshauri, kiongozi na mzee wetu mpendwa Colonel Apson Mwang’onda, mtu ambaye wakati wote wa safari yangu ya kisiasa na uongozi alikuwa msaada mkubwa usiomithilika. Pumzika kwa amani baba"ameandika Bashe 

Mzee Mwang’onda (75) aliaga dunia jana nchini Afrika Kusini.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527