KAMPUNI YA AGGREY & CLIFFORD YANG’ARA TUZO ZA TOP 100 MID-SIZED COMPANIES


Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kampuni ya Aggrey & Clifford, Ibrahim Kyaruzi, akipokea tuzo kwa niaba ya kampuni kutoka kwa Mkurugenzi wa kampuni ya Bankable Tanzania Limited Lawrence Mafuru (Kushoto).

Kampuni ya matangazo na ukuzaji masoko ya Aggrey & Clifford, kwa mara nyingine imepata tuzo kutokana na kuwa miongoni mwa makampuni 100 ya kati yanayofanya vizuri kibiashara.

Kampuni ya Aggrey & Clifford ambayo hivi karibuni ilisherehekea miaka kumi tangu kuanzishwa kwake, ilitunukiwa tuzo hiyo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam kwenye hafla fupi iliyofanyika Serena Hotel.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527