ROGATHE AENDELEA KUOMBA MSAADA WA MATIBABU AMALIZIE DOZI...AWASHUKURU WALIOJITOKEZA MWANZO



Muonekano wa ngozi ya Rogathe Kabla ya kuanza kupatiwa huduma ya matibabu


Muonekano wa ngozi ya Rogathe Kabla ya kuanza kupatiwa huduma ya matibabu


Rogathe Cycprian Makala akionesha namna matibabu yalivyomsaidia kutibu ugonjwa wake wa ngozi kwa fedha za wasamaria wema na sasa hawashwi tena kama hapo awali na anaendelea na masomo yake ya Kidato cha Tano.

Rogathe Cycprian Makala (kushoto) akiwa na mama yake Happines Stephen Makala wakitoka kupatiwa matibabu leo Septemba 2,2019, na kuomba msaada wa fedha ili amalizie matibabu kwa miezi sita iliyosalia na kutoa shukrani wa wasamaria ambao walimsaidia awali na kupata matibabu kwa miezi mitatu.

*****
Happiness Stephen ambaye ni mkazi wa mtaa wa Busulwa kata ya Kitangili Manispaa ya Shinyanga anaendelea kuomba msaada fedha za matibabu kwa binti yake aitwaye Rogathe Cycprian Makala (18), ambaye anasumbuliwa na tatizo la ugonjwa wa ngozi kwa muda wa miaka 16 sasa.

Anatoa shukrani kwa wadau ambao awali waliojitokeza kumsaidia fedha za matibabu kwa binti yake ambazo zimetumika kumtibu kwa miezi mitatu na kusalia miezi sita kwani anatakiwa atibiwe kwa muda wa miezi tisa hivyo anaomba wasamaria wema waendelee kumsaidia ili apate kupona.

Anasema kwa matibau ambayo ameyapata binti yake sasa hivi hali yake inaendelea vizuri hajikuni tena usiku kucha kama hapo awali na anaendelea na masomo yake ya kidato cha Tano kama Kawaida.

Awali kabla ya kupatiwa matibabu binti huyo alikuwa halali usiku kucha anashinda anajikuna tu na hata wakati wa jua kali, huku vipele vikimtoka mwili mzima.

Amesema binti yake huyo kwa sasa anapatiwa matibabu na daktari bingwa kutoka apolo india ambaye hua anakuja mkoani shinyanga kila baada ya mwezi, na matibabu yake yatachukua miezi tisa kwa gharama ya shilingi milioni 4,536,000.

Anasema dozi ya dawa ambayo anatumia kila mwezi ni shilingi 504,000/=, ambapo kwa miezi hiyo tisa ni sawa na shilingi 4,536,000/=.

Kwa yeyote atakaye guswa kumsaidia awasiliane kwa namba zifuatazo:

Vodacom : 0764206669 ukitaka kutuma kwa m-pesa jina litasoma Happines Makala

Tigo: 0676368559, jina litasoma Happines Makala (Tigopesa)

Halotel: 0626845953, jina litasoma Eliud Makala (Halopesa)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527