JESHI LA POLISI IRINGA LAONYA WATAKAOVURUGA MAONYESHO YA UTALII KUSINI

Na Datus Mahendeka, Jeshi la Polisi

JESHI la Polisi Mkoa wa Iringa limewaonya wananchi wa Mkoa huo kuchukua tahadhari wanapotumia barabara hususani kipindi hiki cha Maonyesho ya Utalii Kusini.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamanda wa Polisi, ACP Juma Bwire alisema wakazi wengi wamekuwa wakitumia bararabara bila kufuata tahadhari hali inayoweza kusababisha kugongwa na magari.

” Niwape tahadhari Wananchi pindi wanapotumia barabara ikiwemo kuvuka wasivuke huku wakichat au kuongea na simu, kutakuwa na misafara ya magari hivyo wawe makini” alisema

Alisema Jeshi la Polisi limejipanga kudumisha Ulinzi kipindi chote cha maonyesho hayo huku akitoa wito kwa watumiaji wa vyombo vya moto na nyumba za kulala wageni kudumisha Ulinzi kwenye maeneo yao, kwani mara nyingi kumekuwa na matukio ya upororaji wa kompyuta na mali.

Maonyesho ya Utalii Kusini yanatarajiwa kufunguliwa Septemba 20 na Rais wa Zanzibar na Serikali ya Mapinduzi Do. Ali Muhamed Shein kwenye viwanja wa Kihesa Kilolo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527