WAZIRI MKUU AWAOMBA WAWEKEZAJI KUTOKA NJE YA NCHI KUCHANGAMKIA FURSA TANZANIA

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya muungazo wa Tanzania Kassim Majaliwa amewaomba wawekezaji kutoka nje ya nchi kuchagamkia fursa zilizoko nchini baada ya vikwazo vilivyokuwepo hapo awali kuondolewa.

Waziri mkuu ametoa kauli hiyo jana akiwa mkoani Kagera katika uzinduzi wa wiki ya uwekezaji ambapo amesema kuwa wawekezaji toka nje ya nchi wasiogope kuja kuwekeza hapa nchini kwani tayari fulsa ni nyingi ikiwemo ya viwanda, utalii, madini,na uvuvi .

Amewaomba wawekezaji wajitokeze kwa wingi na kuanza mchakato wa kupitia mfumo wa tehama unaowezesha vitu vingi vya uwekezaji kufanyika kwa njia ya mtandao.

Mkuu wa mkoa Kagera Brigedia Generali Marco Elisha Gaguti amesema maeneo makubwa ya uwekezaji yapo katika sekta za kilimo,utalii,ufugaji,uvuvi,viwanda,misitu,madini na huduma za kijamii.

Wiki ya uwekezaji Kagera iliyoanza august 12 mwaka huu itahitimishwa august 17 mwaka huu ambapo shughuli mbalimbali ikiwemo kutambua maeneo ya uwekezaji ,namna ya kuwekeza yanajadaliwa na wadau ili kuona namna ya kuwekeza katika maeneo hayo.
Na Lydia Lugakila - Malunde1 blog



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527