WAASI WA KIHOUTHI WASHAMBULIA KIWANDA CHA MAFUTA NCHINI SAUDIA ARABIA


Waasi wa kihouthi nchini Yemen hapo jana walifanya Shambulizi la ndege isiyokuwa na rubani dhidi ya kisima cha mafuta cha Shaybah nchini Saudi Arabia kinachotoa takriban mapipa milioni moja ya mafuta ghafi kwa siku.
 

Hilo ni shambulizi la pili la aina hiyo katika sekta hiyo muhimu ya mafuta nchini humo katika siku za hivi karibuni.

Vyombo vya habari nchini humo viliwanukuu maafisa wa serikali ya Saudi Arabia wakisema kuwa uzalishaji mafuta katika kisima hicho haukuathirika Kampuni ya mafuta inayomilikiwa na serikali ya Saudia Aramco, imetoa taarifa inayokiri kutokea moto kiasi katika kituo hicho kinachotoa mafuta huko Shaybah.

Waasi wa kihouthi wamefanya misururu ya mashambulizi ya angani yanayolenga maeneo tofauti tofauti ya Saudi Arabia katika miezi ya hivi karibuni. 

Mzozo huo nchini Yemen kwa kiasi kikubwa unaonekana kuwa ni vita baina ya Saudi Arabia yenye Waislamu wa dhehebu la Kisunni na Iran yenye Waislamu wa madhehebu ya Kishia.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527