WALIOFARIKI KWENYE AJALI YA MOTO MOROGORO WAFIKIA 82

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminieli Aligaesha  amesema  Majeruhi 6 kati ya 38 wa ajali ya moto ya mkoani Morogoro ambao walikuwa wakitibiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, wamefariki Dunia usiku wa kuamkia  leo hospitalini hapo. 




Aminiel amesema Majeruhi waliobaki ni 32 ambapo kati yao  Wagonjwa 17 Wako ICU huku wengine  15 wakiwa Wodi ya Kawaida.

Kwa takwimu hizi mpya zilizotolewa leo, Mpaka sasa idadi ya waliofariki kwenye ajali hiyo  itakuwa imefikia  watu 82.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527