SERIKALI YAAGIZA MASHAMBA MAKUBWA YA TUMBAKU YAPIMWE


Serikali  imeuagiza uongozi wa mkoa wa Tabora kuhakikisha mashamba makubwa ya tumbaku yanapimwa.

Akizungumza na viongozi wa mkoa wa Tabora leo Jumanne Agosti 13, 2019, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi nchini Tanzania, Angelina Mabula amesema kwa kutopimwa mashamba hayo ina maana Serikali  inakosa mapato.

Awali, mkuu wa mkoa wa Tabora, Aggrey Mwanri amemweleza naibu waziri kuwa migogoro ya ardhi mkoani Tabora imepungua kwa kiwango kikubwa kutokana na jitihada mbalimbali zilizofanywa na mkoa pamoja na wilaya kwa kushirikiana na ofisi ya Ardhi kanda ya Magharibi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527