MAHAKAMA YAAMURU USHAHIDI WA VIDEO KESI YA MBOWE NA VIONGOZI WENGINE WA CHADEMA UONYESHWE

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeamuru kuonyeshwa kwa video iliyopokelewa mahakamani hapo kama ushahidi katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema, akiwemo Mwenyekiti wake, Freeman Mbowe, ionyeshwe .


Uamuzi huo umetolewa  Agosti 19, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Thomas Simba, baada ya kupitia hoja za upande zote mbili.

Uamuzi huo unatokana na upande wa utetezi kupinga video hiyo isionyeshwe mahakamani hapo kutokana na upande wa mashtaka kushindwa kuandaa mazingira wezeshi.

Akitoa uamuzi huo, Hakimu Simba alisema sababu zilizotolewa na upande wa utetezi haina mashiko, hivyo video hiyo inatakiwa ionyeshwe katika ukumbi wa Tehama uliopo katika mahakama ya Kisutu.

Hata hivyo hakimu huyo ameiairsha  kesi hiyo kwa muda wa dakika 20 kwa ajili ya maandalizi ya kuangalia video.

Video hiyo inayosemekana ilirekodiwa wakati wa ufungaji wa kampeni za uchaguzi mdogo  wa ubunge wa Kinondoni kwa tiketi ya Chadema Februari 16 mwaka 2018, inadaiwa kubeba matukio yanayomuonyesha Mbowe na wenzake tisa wakiwa kwenye mkutano wa kufunga kampeni za uchaguzi huo, na kwamba ina uhusiano na kesi hiyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527