WATU 63 WAUAWA KWENYE MLIPUKO ULITOKEA KWENYE UKUMBI WA HARUSI


Takriban watu 63 wameuawa na wengine zaidi ya 180 kujeruhiwa jana usiku baada ya kutokea mlipuko wa kujitoa muhanga kwenye ukumbi wa harusi magharibi mwa mji mkuu wa Afghanistan, Kabul.

Ikithitbitisha tukio hilo polisi ya Afghanistan imesema mlipuko ulitokea saa 4.40 usiku ndani ya ukumbi wa harusi wa Shahr-e-Dubai huko Kabul.

Idadi ya vifo huenda ikaongezeka kwani watu kadhaa wapo kwenye hali mahututi.

Hadi sasa hakuna mtu au kundi lolote lililotangaza kuhusika na tukio hilo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527