DEREVA LORI LA MAFUTA LILILOTEKETEA KWA MOTO RUVUMA APATIKANA


Dereva Hurbet Mpete aliekuwa anaendesha lori la mafuta lililopata ajali Mkoani Ruvuma amepatikana akiwa hai.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Simon Marwa  amesema dereva huyo ana michubuko kidogo na amevunjika mbavu, hivyo wamempeleka Hospitali kwa matibabu zaidi.


RPC Marwa amesema uchunguzi zaidi unaendelea kujua chanzo cha ajali hiyo ingawa  shehena ya mafuta lita 33,000 alizobeba zimekutwa salama na mmiliki wa mafuta hayo ameshahamisha.



Lori hilo mali ya James Mwinuka ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Njombe Filling station  lilipata ajali juzi Jumapili Agosti 11,2019 saa 4 usiku  baada ya kuacha  njia na kugonga mti Kijiji cha Hangangadinda mkoani Ruvuma. 



Katika ajali hiyo, kichwa chote cha Lori hilo kiliteketea kwa moto na kubakiza tank pekee lililokuwa na Lita 33, 000 za Petrol.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527