RAIS MAGUFULI AMPA RAIS KENYATTA TAUSI WANNE

Rais Magufuli amemzawadia Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta ndege aina ya tausi kama kumbukumbu ya uhusiano, urafiki na ujirani mwema baina ya nchi hizo mbili.


Magufuli ametoa zawadi hiyo  Jumamosi Julai 6, 2019 wilayani Chato mkoani Geita na kumpatia Kenyatta aliyekuwa nchini Tanzania kwa ziara binafsi ya siku mbili.

“Nimeguswa sijawahi kugawa tausi kwenye nchi yoyote kwa sababu wana historia ya nchi yetu. Kwa  heshima kubwa na mahusiano  yaliyopo kati ya Tanzania na Kenya, nimekubali na hili nataka kulisema wazi.

“Najua watu wataandika lakini hili limenigusa kutoka moyoni, nitatoa tausi wanne watapelekwa Kenya kwa Kenyatta,” alisema Magufuli huku akitabasamu.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527