MWAKYEMBE ATOA ONYO KWA WANAOSAMBAZA PICHA ZA AJALI MITANDAONI

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amewaonya watu wanaopiga picha kwa simu mara tu zinapotokea ajali na kusambaza mitandaoni.

Mwakyembe ametoa onyo hilo leo Jumanne Julai 9, wakati wa shughuli ya kuaga miili ya wafanyakazi wa Azam Media waliofariki jana Julai 8, katika ajali ya gari kati ya Shelui na Igunga na kuongeza kuwa Sheria ya Makosa ya Mitandao inazuia kufanya hivyo.

"Niwaombe Watanzania tuendeleze utamaduni wa utu ndugu zetu wanapopata ajali, niwaombeni acheni tabia ya kupiga picha na kurusha kwenye mitandao, sheria ya mitandao inakataza, hatutazungumza tena hili ni onyo la mwisho" - Waziri Mwakyembe


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post