IRAN YASEMA ITALIPA KISASI KWA UINGEREZA


Mnadhimu mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini Iran Meja Jenerali Mohammad Bagheri amesema leo kwamba, hatua ya Uingereza kuikamata meli yake ya mafuta nje ya eneo la Gibraltar haitapita bila majibu. 

Kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim Bagheri amesema kukamatwa kwa meli hiyo ya mafuta ya Iran chini ya misingi ya visingizio vya kutengenezwa, hakuta pita bila kujibiwa na itakapolazimika Tehran itatoa jibu sahihi. 

Jeshi la majini la Uingereza liliingia katika meli hiyo, Grace 1, nje ya pwani ya Gibraltar siku ya Alhamis na kuikamata kuhusiana na shutuma kwamba inavunja vikwazo kwa kupeleka mafuta nchini Syria. 

Iran imetaka kuachiwa mara moja kwa meli hiyo ya mafuta, wakati kamanda huyo wa jeshi la mapinduzi la Iran ametishia siku ya Ijumaa kukamata meli za Uingereza kwa kulipa kisasi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527