MALI ZA FREEMAN MBOWE KUPIGWA MNADA KESHO


Mali za Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), zinatarajiwa kupigwa mnada Julai 6, mwaka huu.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kampuni ya udalali ya Fosters Auctioneers & General Traders ya jijini Dar es Salaam, mali zitakazopigwa mnada ni kila kitu kilichokuwamo ndani ya Ukumbi wa Bilicanas uliopo Mtaa wa Mkwepu, jijini Dar es Salaam.

“Mnada huo utafanyika kuanzia saa nne asubuhi kwenye ghala la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) karibu na geti namba 3, bandarini,” imesema taarifa hiyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post