HOMA YA DENGUE YAUA WATU 13


Serikali  imesema homa ya dengue imeua watu 13 nchini huku 6,677 wakiugua ugonjwa huo.

Takwimu hizo zimetolewa jana Jumamosi Julai 27, 2019 na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu katika uzinduzi wa mkakati wa Taifa wa kupambana na mbu na wadudu wengineo katika viwanja vya Mnazi Mmoja.

Waziri Ummy alisema awali takwimu zilionyesha vifo sita  lakini Serikali ilifanya tathmini upya na kupata takwimu sahihi..

Alisema ugonjwa huo kwa sasa unapungua kwa maelezo kuwa Juni, 2019 kulikuwa na wagonjwa 536 na tangu kuanzia Julai hadi leo kuna wagonjwa sita pekee.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527