DC MPYA WA IKUNGI AAPISHWA RASMI JIJINI DODOMA

Na.Faustine  Gimu Galafoni,Dodoma.

Mkuu mpya wa Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida   Edward Mpogolo aliyeteuliwa jana usiku na Rais Magufuli ameapishwa leo Julai 25,2019 zoezi lililofanyika   katika makao Makuu ya nchi,Dodoma.

Akizungumza wakati akimwapisha mkuu huyo mpya wa Wilaya  ya Ikungi ,Mkuu wa Mkoa Wa SINGIDA Rehema Nchimbi amesema  amesema amempongeza Mkuu Mpya wa Wilaya ya Ikungi Edward  Mpogolo ambaye kabla ya uteuzi huo alikuwa katibu tawala wilaya ya Dodoma Mjini.

Hivyo, Mhe.Nchimbi amemtaka mkuu huyo mpya wa wilaya kutekeleza  majukumu yake katika miradi mbalimbali ya wilaya ya Ikungi ili kuwaletea  Maendeleo ya Wananchi.

“Singida ni makao makuu mwenza   ya Tanzania ,sasa  wewe mkuu wa wilaya Edward  Mpogolo ni kuwahakikishia watanzania kuwa Singida sio kame,Singida sio masikini,Singida sio njaa.Singida imekuwa ikipokea fedha  nyingi kama mikoa mingine kwani kwa ndani ya miaka minne imepokea zaidi ya Tsh.bilioni mia saba kwa ajili   ya Maendeleo “alisema Nchimbi.

Aidha ,Mkuu huyo wa Mkoa Wa Singida amemtaka   mkuu mpya wa Wilaya ya Ikungi kwenda kusimamia mkakati kabambe wa Mkoa Wa Singida ambao umeanzishwa kwa lengo la kupunguza kero za mishahara kwa watumishi ujulikanao kama”Mshahara wangu Uko wapi “huku pia akimtaka kwenda kutatua na kusimamia suala la kilimo hususan kilimo cha Alizeti na korosho Pamoja na Sekta ya kilimo.

Kwa  upande wake  Mkuu mpya wa wilaya ya Ikungi Edward  Mpogolo ameahidi kuwa ataenda kushirikiana na halmashauri ya Ikungi katika kusimamia miradi mbalimbali na kuongeza makusanyo ya halmashauri   ili kwa ajili ya Maendeleo ya nchi katika utekelezaji wa Ilani ya  Uchaguzi ya Mwaka 2015.

Kabla ya uteuzi huo, Bw. Mpogolo alikuwa Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma, nafasi ya Katibu Tawala wa Wilaya ya Dodoma itajazwa baadaye.

Ikumbukwe kuwa  hapo jana Julai 24,2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli alimteua Bw. Edward Mpogolo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida ambapo Mpogolo anachukua nafasi ya Bw. Miraji Mtaturu ambaye amechaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki lililokuwa linaongozwa na Tundu Lisu [CHADEMA ]ambapo umbunge wake ulifutwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527