RAIS WA TUNISIA CAID ESSEBSI AFARIKI DUNIA


Rais wa Tunisia, Beji Caid Essebsi amefariki dunia leo Alhamisi Julai 25, katika hospitali  ya  kijeshi mjini  Tunis akiwa na umri wa miaka 92, baada ya kuugua kwa kipindi kirefu.

Taarifa zinasema Essebsi alipelekwa  hospitalini hapo jana jioni kwa  mara ya pili  ndani ya mwezi mmoja.

Rais huyo alikuwa kiongozi mkongwe zaidi duniani baada ya Malkia Elizabeth II wa Uingereza na amekuwa  madarakani  tangu  mwishoni mwa mwaka 2014 baada ya kushinda uchaguzi huru wa kwanza kufuatia vuguvugu la maandamano katika mataifa ya kiarabu.

Mapema mwaka huu, Essebsi alitangaza kwamba hatogombea katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa Novemba mwaka huu alisema kwamba muda umewadia kwa kijana kushika nafasi hiyo ya uongozi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527