Picha : HAWA NDIYO WAFANYAKAZI WA AZAM TV WALIOFARIKI KWENYE AJALI SINGIDA

Wafanyakazi watano wa kampuni ya Azam Media wamefariki dunia leo Jumatatu Julai 8, 2019 katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Shelui mkoani Singida baada ya gari aina ya Coaster walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori.

Mkurugenzi wa uzalishaji vipindi wa kampuni hiyo, Yahya Mohamed amewataja waliofariki dunia kuwa ni Salim Mhando, Florence Ndibalema, Said Haji, Sylvanus Kasongo na Charles Wandwi.

Mbali na wafanyakazi hao, watu wengine wawili wamefariki dunia katika ajali hiyo ambao ni madereva wa Coaster lililokuwa limewapakia wafanyakazi 10 wa kampuni hiyo, pamoja na dereva wa lori.

Wafanyakazi hao walikuwa wakielekea wilayani Chato Mkoa wa Geita katika uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Chato-Burigi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527