VANESSA MDEE ATANGAZA RASMI KUACHANA NA JUMA JUX


Msanii wa Bongo Fleva Vanessa Mdee ametangaza rasmi kupitia Instagram story yake kuwa ameachana na aliyekuwa mpenzi wake Juma Jux baada ya shabiki kuuliza kama wameachana   na Jux.

Vanessa Mdee alijibu ‘Ndio, lakini ni marafiki wazuri sana na tutabaki kuwa familia daima’ swali hilo limekua likionekana kutojibiwa mara nyingi endapo wawili hao wakiulizwa kuhusu penzi lao kuvunjika, siku kadhaa zilizopita Mimi Mars ambaye ni mdogo wake Vanessa aliweka wazi kuwa Jma na Vee wameachana na wamebaki kama marafiki.

Juma Jux pamoja na Vanessa walianza mahusiano yao miaka kadhaa iliyopita na August 2017 walitengana lakini ndani ya mwaka huo huo wa 2017 walirudiana rasmi juu ya stage kwenye tamasha la Fiesta lilofanyika Dar Es Salaam.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527